Mbweha alikuwa akitafuta chakula nyikani wakati alipomuona mbuzi kileleni juu ya mwinuko
akila majani.
Kwa kuwa mwenyewe alikuwa hawezi kupanda kule juu alifikiria namna ya kufanya mbuzi ateremke na kuja chini ili amle.
Akamwita mbuzi na kumwambia:
"Samahani mwenzangu mbuzi," akasema kwa sauti ya upole," ni hatari sana kukaa mahala kama hapo ulipo. Shuka chini kabla hujaumia. Isitoshe majani hapa chini ni laini na matamu zaidi kuliko hayo ya huko juu. Sikiliza ushauri wangu na ushuke chini kwa usalama wako."
Hata hivyo mbuzi alimfahamu mbweha fika na nia yake mbaya.
"Nenda zako hayawani wee. Haujali chochote kuhusu usalama wangu. Na wala hujali kama ninakula majani mazuri au mabaya. Nia yako ni kutaka mimi nishuke ili unile tu! Umefulia leo! Ishilia zako!"
Adili au somo la hadithi: Kuwa na mashaka na ushauri 'mzuri' toka kwa adui yako.
Hafeez Sammy na Shukrani: Simulizi za Aesop.
Sunday, March 15, 2009
Subscribe to:
Posts (Atom)
